KATIKA MICHUANO YA AFCON GHANA NA DRC WAMETOKA DROO YA 2-2


Kikosi cha DRC

Hatimaye michuano ya Fainali za Kombe la Afrika, AFCON inayofanyika nchini Afrika Kusini imeanza kuzaa magoli. Mechi ya kwanza ya kundi B kati ya Ghana na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, imemalizika kwa kufungana magoli 2-2.
Wachezaji wa Ghana
Ghana ilianza kufunga kupitia kwa Emmanuel Agyemang Badu katika dakika ya 40. Kipindi cha pili kilianza kwa Ghana tena kuongeza goli la pili likifungwa na Kwadwo Asamoah katika dakika ya 49.
Tresor Mputu ambaye ni ni nahodha wa timu ya DRC alifunga bao la kwanza katika dakika ya 53. Goli la pili la DRC limepatikana kwa njia ya mkwaju wa penalti ukifungwa na Dieumerci Mbokani dakika ya 69. Kwa matokeo hayo timu hizo zimegawana pointi moja moja.
Mechi ya pili ya kundi B inazikutanisha Mali na Niger.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget