Taarifa zinasema Bw Kaweesi ameuawa baada ya gari lake kumiminiwa
risasi na watu wasiojulikana alipokuwa anaondoka kwake nyumbani
Kulambiro, Kisaasi kaskazini mashariki mwa mji mkuu Kampala.
Walinzi wake wawili walioandamana naye pia wameuawa.
Bw Kaweesi aliteuliwa kuwa msemaji wa polisi Agosti mwaka jana.
Taarifa
zinasema alikuwa njiani kwenda kuwahutubia wanafunzi katika chuo kikuu
cha Uganda Christian University alipokumbana na mauti yake. Wanafunzi
walikuwa tayari wamekusanyika ukumbini katika chuo hicho.
Miili ya watatu hao imepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mulago
source bbcswahili
picha hii ni kwa Hisani ya Izabreez.blogspot.com
Post a Comment