Kundi la Daesh lajaribu kujipenyeza Libya


Kundi la Daesh lajaribu kujipenyeza Libya Gazeti moja la nchini Libya limeandika kuwa, kundi la magaidi wa kitakfiri wa Daesh linajaribu kila linalowezekana ili kujipenyeza huko Libya na kupanua maovu yake nchini humo. Gazeti la Buabatul Wasat limeandika kuwa, maafisa wa idara za kiintelijenisia za Tunisia, Misri na Algeria walikutana juma hili ili kuchunguza ripoti za kiusalama na kutafuta njia za kuzuia kuenea kwa harakati za kigaidi za kundi la Daesh katika eneo.  
 Gazeti hilo limevinukuu vyombo vya kiusalama na kuandika kuwa tetesi zilizopo zinaonyesha kuwa, baadhi ya Walibya wenye misimamo ya kufurutu ada wanarejea nchini humo na kujaribu kuasisi kambi kwa ajili ya kundi la Daesh huko kaskazini mwa Afrika. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Kukosekana serikali kuu yenye nguvu huko Libya tangu kung’olewa madarakani dikteta Muammar Gaddafi mwaka 2011 huenda kukaandaa mazingira ya kupanuka kwa harakati za kundi la kitakfiri la Daesh nchini humo.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget