Watu 29 wauawa kwenye machafuko mapya Kenya

Kwa akali watu 29 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa, baada ya watu wanaobeba silaha kufanya mashambulio katika maeneo mawili tofauti katika Kaunti za Lamu na Tana River, Pwani ya Kenya. Mwenda Njoka Msemaji wa Wizara ya Usalama wa Ndani wa Kenya amesema kuwa, wanamgambo wanaobeba silaha walilishambulia eneo la Hindi, lililoko umbali wa kilomita 15 kutoka Kaunti ya Lamu na kuuawa watu tisa. Njoka ameongeza kuwa, watu wengine 20 waliuawa kwenye shambulio lililofanywa katika eneo la Gamba lililoko karibu na Kaunti ya Tana River. Wakati huohuo, Abdulaziz Abu Musab Msemaji wa al Shabab amesema kuwa, kundi hilo ndilo lililohusika na shambulio hilo. Kwa upande mwingine William Ruto Naibu wa Rais wa Kenya amevitaka vyombo vya usalama kuwasaka na kuwatia mbaroni watekelezaji wa shambulio hilo. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Grace Kaindi Naibu Inspekta wa Jeshi la Polisi la Kenya amelituhumu kundi la Mombasa Republican Council MRC kuwa ndilo lililohusika na shambulio hilo ambalo linatajwa kuwa linalotokana na msukumo wa kisiasa, kidini au mgogoro wa ardhi. 

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget