SOMA HAPA JINSI WASANII WA FILAMU WATAKAVYOMUENZI MSANII WA FILAMU MAARUFU NCHINI STEAVIN KANUMBA APRILI SABA MWAKA HUU


SOMA HAPA JINSI WASANII WA FILAMU WATAKAVYOMUENZI MSANII WA FILAMU MAARUFU NCHINI STEAVIN KANUMBA APRILI SABA MWAKA HUU



WASANII wa filamu Tanzania wapo katika harakati za mwisho wa mchakato wao katika maandalizi ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba, ikiwa ni moja ya jambo walilokusudia kuhakikisha wanamuenzi na kuthamini mchango aliouacha kwenye tasnia ya filamu

Akizungumzia maandalizi hayo jijini Dar es Salaam rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifwamba alisema kuwa baadhi ya maandalizi yameanza kwa ajili ya kumuenzi marehemu Kanumba, huku wakishirikiana na familia ya marehemu ili kuweka mipango ya nini kifanyike katika harakati za kutimiza lengo
Alisema kuwa lengo lao lazima litimie kwa sababu walikusudia kufanya kitu kwa ajili ya kumuenzi marehemu kutokana na mchango wake aliouacha kwenye filamu na ili kudhihirisha hilo wanaamua kumenzi katika hali ya kiupekee
"Lazima tufanye kitu cha tofauti katika kumuenzi marehemu na ili tuonyeshe upendo wetu lazima tuheshimu kile alichokiacha kwa kuendeleza" alisema Mwakifwamba
Aliongozea kuwa muda ukifika na maazimio yakipitishwa ndipo ataweka wazi ni jambo gani lililokusudiwa kufanyika
Marehemu Steven Kanumba amefariki april 7 mwaka 2012 ambapo chanzo cha kifo chake kinadaiwa kuwa ni ugomvi wa mapenzi, na aliyekuwa mpenzi wake msanii mwenzie wa filamu  Lulu

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget