Watoto wafunzwa fikra za Osama Pakistani

Kiongozi wa kidini nchini Pakistani anatoa mafunzo ya fikra za Osama bin Laden kwenye shule za dini kwa Wanafunzi takriban 5,000.ingawa serikali ya nchi hiyo inapambana na wanamgambo wa Taliban kaskazini magharibi mwa Pakistani, haina mipango ya kuzifungia shule zinazotoa elimu kwa watoto kuunga mkono wanamgambo wa Taliban.
Imamu wa msikiti mmoja mjini Islamabad Abdul Aziz Ghazi amesema wana malengo sawa na Taliban lakini amesema hawatoi mafunzo ya kijeshi.
Kiongozi huyo amesema wanatoa mafunzo kuhusu misingi ya Jihad ila ni juu ya wanafunzi kupata mafunzo ya kijeshi baada ya kutoka shuleni hapo.
Ghazi anamiliki shule nane za kidini yaani Madrasa,moja ya shule yake iliwahi kufanya ziara ya kwenda kukutana na Osama Bin Laden nchini Afghanistan.
Hivi sasa wasichana 3,000 na wavulana 2,000 wanasoma kwenye taasisi zake.
Mitaala ya shule zake inatoa mafunzo ya kusoma Quran, kiarabu na thiolojia,hesabu na sanaa inaonekana kuwa masomo ya kidunia, vitabu vingi vimeandikwa na Ghazi na kuchapishwa katika shule hizo zenye vyumba vya kuchapisha.
Katika moja ya shule, kuna maktaba iliyopewa heshima ya jina la bin Laden .

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget