Buriani kwa Rais Michael Sata Zambia

 
Mwili wa hayati Rais Michael Sata utazikwa leo mjini Lusaka Zambia
Mazishi ya kitaifa yanafanyika nchini Zambia kumuaga hayati Rais wa nchi hiyo Michael Sata aliyefariki hospitalini mjini London Uingereza mwezi jana.
Sata alikuwa na umri wa miaka 77.
Katika wiki chache zilizopita, wanachi wamekuwa wakitoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi huyo ambaye mwili wake ulikuwa umelazwa katika majengo ya bunge.
Rais Sata alifariki akipokea matibabu mjini London Uingereza
Mazishi yanayofanyika mjini Lusaka yatahudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kikanda.
Rais Sata atazikwa katika eneo lenye makaburi yaliyotengewa Marais wa nchi hiyo.
Taifa hilo kwa sasa linaongozwa na kaimu Rais huku uchaguzi mkuu ukipangwa kufanyika katika muda wa miezi michache ijayo.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget