Serikali Tanzania ichunguze kashfa ya pembe za ndovu

Serikali Tanzania ichunguze kashfa ya pembe za ndovuSerikali ya Tanzania imetakiwa ifanye uchunguzi wa kimataifa kubaini watu waliohusika na ripoti iliyoitia doa serikali kuhusu madai ya kusafirishwa pembe za ndovu kwenye ndege ya Rais wa China, Xi Jinping. Kauli hiyo imetolewa Bungeni na Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi wakati akichangia mapendekezo ya utekelezaji wa mpango wa taifa kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Mbunge huyo wa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA amesema kuwa, serikali isije na kauli nyepesi kama ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuwa taarifa hizo ni za uzushi na badala yake ifanye uchunguzi. Akizungumza hivi karibuni katika mahojiano maalumu na idhaa hii ya Radio Tehran, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Upinzani cha Wananchi CUF alielezea kusikitishwa kwake na mitandao ya ufisadi na ujangili iliyokita mizizi serikali na kubainishwa kwamba, umefika wakati sasa kwa Watanzania kuleta mabadiliko ya uongozi ili kuokoa utajiri na rasilimali za nchi zinazoporwa huku serikali ya chama tawala CCM ikionekana kushindwa kukabiliana na wimbi hilo la uporaji.

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget