WARIOBA: Katiba pendekezi haijakidhi vigezo



Baadhi ya wajumbe waliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba wameitaka serikali ichapishe kwa wingi na kuzisambaza kwa wananchi nakala za katiba pendekezwa, ili wananchi waisome na kuielewa kabla ya kuipigia kura ya maoni.  
Wakizungumza katika mdahalo ulioandaliwa na mfuko wa MWALIMU NYERERE uliofanyika JIJINI DAR ES SALAAM, wajumbe hao akiwemoaliyekuwa mwenyekiti wa tume hiyo jaji mstaafu JOSEPH SINDE WARIOBA, wameelezea kutoridhishwa na tunu za taifa haki za makundi mbalimbali kama vile watu wenye ulemavu, wanawake na watoto pamoja  na baadhi ya vipengele kuondolewa,
Akizungumza katika mdahalo huo, aliyekuwa mjumbe wa tume BW HAMFREY POLEPOLE ametaka kuwepo maridhiano ya kikatiba kati ya pande mbili za muungano ili uwepo muungano unaokubaliwa, unaodumishwa na kulindwa kikatiba huku akieleza kusikitishwa na kitendo cha kufutwa kwa ibara muhimu zilizokuwa katika rasimu ya katiba na kushauri ibara hizo zirejeshwe kwani ndiyomsingi wa katiba inayozingatia maslahi ya wananchi na taifa imara.

Hata hivyo mdahalo huo umekuwa na ulinzi mkali wa polisi tofauti na midahalo mingine ambapo mwandishi alishuhudia wahudhuriaji wakiwa wanakaguliwa na vifaa maalum kabla ya kuingia ndani.,

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget