Koreas Kaskazini
imeishutumu Marekani kwakusambaza makusudi virusi vya ugonjwawa Ebola na kwamba inatengeneza
silaha hiyo yakibailojia ili kuwa taifa lenye nguvu zaididuniani
Taifa hilo limelazimika kufunga mipaka yakekuzuia watalii ikiwa ni pamoja na kumtenga kila anayeingia. Ripoti ya Korean Central News Agency (KCNA) inadai kuwa aliyekuwa msaidizi wa Rais wa zamani wa Marekani, Reagan amewataarifu kuwa Marekani ilivumbua seli ya kirusi cha Ebola kwa malengo ya kuanzisha silaha ya kibailojia.
Msaidizi huyo alitajwa kwa jina la Roberts,
ambaye gazeti la The Washington Post
limesema anaweza kuwa Paul Craig Roberts.
Hivi karibuni Roberts aliandika makala kwenye
blog isemayo: ‘Is The US Government The
Master Criminal Of Our Time?’ Makala hiyo
ilisema kuwa Marekani ilitoa dola milioni 140
kwenye kampuni moja ya dawa kufanya utafiti
wa kirusi hicho na kuchagua bara la Afrika
kama sehemu ya majaribio.
Makala hiyo ilisema taarifa hiyo ilitolewa na
profesa wa Liberia ambaye hakutajwa jina.
Iliongeza kuwa Marekani ilitengeneza kinga ya
kirusi hicho lakini ilizuia kujulikana duniani
kwa faida yake yenyewe.. sourse, mpekuzi
Post a Comment