Mwandishi TV1 Arusha anaongoza kwa kuomba pesa kwa viongozi

Mwandishi Jeny Edward anayeripoti kituo cha TVI hapa Arusha amegeuka mwiba kwa viongozi wa ngazi mbalimbali serikalini wakiwemo mawaziri,kwa kuwakwida wampatie fedha wanapokuwa kwenye ziara mbalimbali za kikazi huku akitumia kivuli cha kuwafanyia interview.
Mfano halisi ni juzi waziri mkuu,Mizengo Pinda alipokuwa kwenye kongamano la nyuki jijini Arusha,bila aibu akiwa na mwenzake alimfuata hadi chumbani alikofikia katika hotel moja maarufu hapa mjini na kumlazimisha ampatie fedha huku akimweleza kuwa yeye hakulipwa kwenye mkutano huo.

Kana kwamba haitoshi waziri Nyalandu naye alipata joto hilo hilo kwa kufuatwa kwenye sehemu ya kupumzikia katika jengo la mikutano AICC akitakiwa ampatie fedha ,Nyalandu pamoja na kujitetea kuwa hawezi kutoa hela hadharani ,alilazimika kuongozana na mwandishi huyo hadi kwenye gari lake na kumpatia mshiko wake.

Mimi kama afisa habari wa wizara nilisikitishwa sana na tabia hiyo hasa baada ya kuelezwa kuwa ndiyo tabia yake iliyojengeka ya kuwaomba fedha mawaziri,najua hii tabia ipo sana hapa Arusha lakini nimeambiwa huyu ndo kinara wao ,naomba chama cha wanandishi wa habari Arusha APC walishughulikie suala la maadili jambo hilo sio jema,mbaya zaidi alimwagia matusi ya nguoni mbele yangu mwakilishi wa habari na maelezo wa mkoani Arusha, Prisca Libaga baada ya kumfuata na kumhoji tabia ya kuwazonga viongozi hadi kwenye magari akitaka wampatie fedha.hisani jamiiForum

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

designed by izack. Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget